• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
MISSENYI DISTRICT COUNCIL
MISSENYI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Missenyi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Missenyi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni na Vitengo
      • Divisheni ya Utawala na Usimamizi Rasilimali Watu
      • Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Divisheni ya Maendeleo ya Jamii
      • Divisheni ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Divisheni ya Elimu Sekondari
      • Divisheni ya Miundombinu na Maendeleo ya Vijiji
      • Idara ya Ardhi na Maliasili
      • Divisheni ya Mipango na Uratibu
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Huduma za Manunuzi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Sanaa, Utamaduni na Michezo
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Watalii
    • Kilimo
    • Uvuvi
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Madiwani
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Kiuchumi
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Kudhibiti ukimwi
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayo Tekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Uviko19
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha mbalimbali

ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA MISSENYI KATIKA KATA ZOTE 20

Posted on: March 7th, 2023

Mh. Mkuu wa Wilaya ya Missenyi Kanali Wilson Sakulo ameanza ziara yake leo terehe  07 Machi 2023 katika kata ya Ruzinga ambapo anatarajia kuzunguka katika kata zote 20 za halmashauri ya wilaya ya Missenyi ili kusikiliza na kutatua kero za wananchi kupitia mikutani ya hadhara.

Katika ziara hizo Kanali Sakulo ana ambatana na Kamati ya Usalama ya Wilaya, wataalamu mbalimbali kutoka taasisi za serikali kama vile TARURA, RUWASA, TFS na TANESCO pamoja na wakuu wa Divisheni na Vitengo kutoka Halmashauri ya Missenyi.

Katika ziara zake kwa kila kata ameaandaa utaratibu wa kufanya vikao vya ndani na watumishi wote ili kusikiliza na kutafuta ufumbuzi wa mambo mbalimbali wanayokutana nayo wakiwa kazini kutekeleza majukumu yao ya kisheria.

Akiwa katika Kata ya Ruzinga katika mkutano wa hadhara uliofanyika kati uwanja wa Umultunga uliopo nje ya ofisi ya Kata aliweza kusikiliza kero mbalimbali pamoja na kuzitolea ufumbuzi katika mkutano huo.

Baadhi ya mambo yaliyo ulizwa na wanachi walio wengi ni pamoja na kupelekwa umeme katika kitongoji cha  Busheza Kijiji Ruhija na baadhi ya maeneo mengine, Huduma ya Maji katika kata ya Ruzinga, Badhi ya barabara kuomba kufanyiwa matengenezo, utaratibu wa uuzwaji ardhi, manufaa ya hewa ya ukaa, mgogoro wa ardhi baina ya waislamu na Mzee Kamara, Pamoja na masuala ya utawala bora katika maneo ya vijiji haswa katika kufanya mikutano kwa mujibu wa taratibu za kisheria pamoja na wananchi kupewa haki ya kusikilizwa katika mikutano hio.

Maswali yote yalitolewa ufafafanuzi yakiwemo ya umeme ambapo kanali Sakulo alisema "Mhe. Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan anajitahidi kuhakikisha vijiji vyote vitatu vilivyo salia katika wilaya ya Missenyi vinapata umeme kisha awamu ya vitongoji itafuata hivyo wananchi wa Busheza wawe wavumilivu."

Mkuu wa Jeshi la Polisi Missenyi Marwa Mwita aliwasihi wananchi wa Ruzinga kuhakikisha wanafuata taratibu za sheria kwani kumekua na wananchi wanao anzisha maandamano bila kuomba kibali polisi na maandamano kama hayo ni batili.

Kwa upande wake mwenyekiti wa chama cha mapinduzi kata ya ruzinga Bw. Joseph Kamara alishukuru ujio wa mkuu wa wilaya kwani umesaidia sana katika kuleta suluhu ya mambo mengi kwa wananchi wa Ruzinga pamoja na kumuomba mkuu wa wilaya kurudi tena Ruzinga wakati mwingine.

Aidha wanachi wakati wakiwasilisha kero zao walimpongeza mkuu wa wilaya kwa kupanga ratiba ya kuwatembelea wananchi wake kwa kuwafikia walipo na kusikiliza kero na maono yao kwani wananchi walio wengi wanashindwa kufika wilayani kutokana na umbali.

Ziara hii imeanza kwa tarafa ya kiziba na hapo baadae itahamia katika tarafa ya missenyi na kata inayofuatia ni Kata ya Kitobo mnamo tarehe 09 Machi 2023 na Ziara katika tarafa ya Kiziba inatarajiwa kukamilika tarehe 23/03/2023 katika Kata ya Byango.

Tarifa Kwa Umma

  • TANGAZO LA MABADILIKO YA TAREHE YA UCHAGUZI MDOGO WA SERIKALI ZA MITAA MWAKA 2023 March 06, 2023
  • WITO KWA WAZAZI NA WALEZI KUWAPELEKA WATOTO SHULENI January 07, 2023
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2022 January 29, 2023
  • TANGAZO LA UCHAGUZI MDOGO WA SERIKALI ZA MITAA WA MWAKA 2023 March 02, 2023
  • Tazama zote

Habari mpya

  • USHIRIKISHWAJI WA WANANCHI WABORESHA MAZINGIRA YA KUJIFUNZIA SHULENI

    March 10, 2023
  • DC MISSENYI : NAWAAGIZA VYOMBO VYA DOLA KUHAKIKISHA MNAZUIA UKATILI WA KIJINSIA.

    March 08, 2023
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA MISSENYI KATIKA KATA ZOTE 20

    March 07, 2023
  • ZIARA YA MADIWANI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MISSENYI KATIKA WILAYA YA KYERWA

    February 16, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • JINSI YA KUOMBA MKOPO KUTOKA BODI YA MKOPO
  • Sheria ndogo za Halmashauri

Tovuti Muhimu

  • Tovuti ya Mkoa Kagera
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Tovuti ya Serikali Kuu
  • Tovuti ya TAMISEMI

Watembeleaji walipo

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Anuani zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki @2017 Wilaya ya Missenyi. Haki zote zimehifadhiwa