• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
MISSENYI DISTRICT COUNCIL
MISSENYI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Missenyi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Missenyi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni na Vitengo
      • Divisheni
        • Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi
        • Divisheni ya Elimu Sekondari
        • Divisheni ya Mipango na Uratibu
        • Divisheni ya Miundombinu na Maendeleo Vijijini na Mjini
        • Divisheni ya Utawala na Usimamizi Rasilimali Watu
        • Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
        • Divisheni ya Maendeleo ya Jamii
        • Divisheni ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
        • Divisheni ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Vitengo
        • Kitengo cha Sanaa, Utamaduni na Michezo
        • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
        • Kitengo cha Huduma za Kisheria
        • Kitengo cha TEHAMA
        • Kitengo cha Maliasili na Hifadhi ya Mazingira
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
        • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
        • Kitengo cha Huduma za Manunuzi
        • Kitengo cha Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
    • Tarafa
      • Tarafa ya Missenyi
        • Kata ya Mutukula
        • Kata ya Minziro
        • Kata ya Nsunga
        • Kata ya Kakunyu
        • Kata ya Kassambya
        • Kata ya Kyaka
        • Kata ya Mushasha
        • Kata ya Kilimilile
        • Kata ya Mabale
        • Kata ya Bugorora
      • Tarafa ya Kiziba
        • Kata ya Bugandika
        • Kata ya Kitobo
        • Kata ya Buyango
        • Kata ya Ruzinga
        • Kata ya Bwanjai
        • Kata ya Gera
        • Kata ya Ishozi
        • Kata ya Ishunju
        • Kata ya Kanyigo
        • Kata ya Kashenye
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Kiuchumi
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Kudhibiti ukimwi
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayo Tekelezwa
    • Miradi Inayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha

WIKI YA KAGERA -UJUMBE KUTOKA AFRIKA MASHARIKI NA KATI

Posted on: August 15th, 2019

Wiki ya Uwekezaji Kagera imeanza rasmi mkoani Kagera Agosti 12, 2019 kwa Mabalozi kutoka nchi za ukanda wa Afrika mashariki na kati kueleza fursa zinazopatikana katika nchi walizotoka na namna gani wafanyabiashara wa Kagera na Kanda ya Ziwa wanaweza kuchangamkia fursa hizo.

Mabalozi hao waliwasilisha fursa mbalimbali kwa wafanyabiashara wa mkoa wa Kagera waliohudhuria kongamano kwa lengo la kuwaonyesha fursa zinazopatikana katika nchi walizopo. Mabalozi wa Tanzania kutoka katika nchi za Uganda, Rwanda, Burundi, Kenya pamoja na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wamehuzuria kongamano.

Akiwasilisha fursa zinazopatikana Rwanda balozi wa Tanzania Nchini humo Inspekta Jenerali Mstaafu Ernest Mangu ameushauri Mkoa wa Kagera kujenga masoko ya mipakani ili kusogeza bidhaa mbalimbali zinazopatikana nchini kuyafikia masoko ya nchi jirani haraka tofauti na ilivyo sasa kwani wafanyabiashara kutoka nchi za nje wamekuwa wakiingia ndani na kujitafutia bidhaa wenyewe.

Katika hatua nyingine balozi wa Tanzania Nchini Kenya Dk. Pindi Chana alisema kuwa wafanyabiashara wa Kagera na Tanzania bado wanahitaji Elimu kubwa juu ya biashara za kimataifa huku akitilia mkazo matumizi ya teknolojia za mitandao katika biashara zao badala ya kubeba bidhaa na kwenda kutafuta soko.

Mhe. Dk. Aziz P. Mlima balozi wa Tanzania nchini Uganda amewataka wakulima na wafanyabiashara wa mkoa wa Kagera kulima zao la parachichi ambalo sasa lina soko kubwa nchi za nje kuliko kujikita kupanda miti ya mbao pekee.

Kaimu Balozi wa Tanzania nchini Burundi Dr. Edmund Kitokezi amewataka wafanya biashara nchini kutoiangalia Burundi kwa udogo wake kwani fursa za kibiashara zilizopo Burundi ni nyingi.

Naye Balozi wa Tanzania nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Lt. Jen. (mst) Paul I. Mella amewashauri wafanya biashara wa Mkoa wa Kagera na Tanzania kwa ujumla kutumia ukubwa wa eneo na wingi wa watu nchini Kongo kama fursa ya pekee nchini humo. “nchi ya Kongo ina soko kubwa la biashara na si mkoa wa Kagera tu bali Kanda ya ziwa kutokana na ukubwa nchi  na wingi wa watu” alisema Lt. Mella.

Wakati huo huo Mwenyekiti wa Kongamano la wafanyabiashara ambae pia ni Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco E. Gaguti amewataka wafanayabiashara wa Kagera kuchangamkia fursa mbali mbali za biashara. “Hapa tunaongelea fursa ya kitaifa na si mkoa wa Kagera tu kwani kati ya nchi nane zinazopakana na Tanzania nchi nne zote zinapakana na Mkoa wa Kagera kwa hiyo mkoa huu ni kitovu cha uchumi wa Nchi za Afrika Mashariki na Kati nataka kuona hamasa ya wafanya biashara wetu hapa wakitumia fursa hiyo.” Alisistiza MKuu wa Mkoa Gaguti

Naye Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Bw. Amon Mpanju hakusita kutoa aliyo nayo kwa wafanya biashara wa mkoa wa kagera huku akiwataka wachangamkie fursa ya uongozi awamu ya tano chini ya Rais John Pombe Joseph Magufuri ambao ni rafiki kwa wawekezaji wa ndani na nje ya nchi. “Mkoa wa Kagera sasa ni wakati wake wa kuinuka kiuchumi katika Awamu hii ya Tano na uongozi wa Mkoa usiruhusu malumbano ya kiasiasa kukwamisha maendeleo pia usiruhusu wafanyabiashara wabinafsi kuhodhi biashara wao peke yao” alisisitiza Mh Mpanju.

Akitoa shukrani kwa mabalozi hao kuja katika kongamano Mbunge wa Bukoba Mjini Mh. Wilfred Lwakatare amesema mabalozi hao ni sawa tu wametoa cheki ya fedha iliyo wazi kwa wafanya biashara na wananchi kwa ujumla na kilichobaki ni wao tu (wafanya biashara) kuandika kiasi chochote cha fedha wanachohitaji.

Tarifa Kwa Umma

  • TANGAZO LA KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA WILAYANI MISSENYI April 14, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO MAADHIMISHO YA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI MACHI 8,2025 March 06, 2025
  • TANGAZO LA UTOAJI WA HUDUMA ZA UZAZI WA MPANGO WILAYANI MISSENYI March 03, 2025
  • TANGAZO LA MKUTANO WA KAWAIDA WA BARAZA LA MADIWANI WA ROBO YA PILI YA MWAKA 2024/2025 February 24, 2025
  • Tazama zote

Habari mpya

  • WALIOKOSA MIKOPO KWA AWAMU YA KWANZA WAPEWE ELIMU

    April 30, 2025
  • WANANCHI MISSENYI WAASWA KUENZI MUUNGANO KWA VITENDO

    April 26, 2025
  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YAJIRIDHISHA NA UTARATIBU WAKUBADILI JINA LA JIMBO LA UCHAGUZI NKENGE

    April 25, 2025
  • 60% YA MAPATO YA NDANI INAPELEKWA KWENYE MIRADI YA MAENDELEO

    April 24, 2025
  • Tazama zote

Video

HALMASHURI YATOA VITI MWENDO NA FIMBO NYEUPE KWA WALEMAVU
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Sheria ndogo za Halmashauri

Tovuti Muhimu

  • Tovuti ya Mkoa Kagera
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Tovuti ya Serikali Kuu
  • Tovuti ya TAMISEMI

Watembeleaji walipo

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Missenyi

    Sanduku la Posta: 38 Kyaka - MISSENYI

    Namba ya Simu ya mezani: +255 28 298 2836

    Namba ya simu : +255 28 298 2836

    Barua pepe: ded@missenyidc.go.tz

Anuani zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki @2017 Wilaya ya Missenyi. Haki zote zimehifadhiwa