• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
MISSENYI DISTRICT COUNCIL
MISSENYI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Missenyi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Missenyi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni na Vitengo
      • Divisheni
        • Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi
        • Divisheni ya Elimu Sekondari
        • Divisheni ya Mipango na Uratibu
        • Divisheni ya Miundombinu na Maendeleo Vijijini na Mjini
        • Divisheni ya Utawala na Usimamizi Rasilimali Watu
        • Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
        • Divisheni ya Maendeleo ya Jamii
        • Divisheni ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
        • Divisheni ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Vitengo
        • Kitengo cha Sanaa, Utamaduni na Michezo
        • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
        • Kitengo cha Huduma za Kisheria
        • Kitengo cha TEHAMA
        • Kitengo cha Maliasili na Hifadhi ya Mazingira
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
        • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
        • Kitengo cha Huduma za Manunuzi
        • Kitengo cha Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
    • Tarafa
      • Tarafa ya Missenyi
        • Kata ya Mutukula
        • Kata ya Minziro
        • Kata ya Nsunga
        • Kata ya Kakunyu
        • Kata ya Kassambya
        • Kata ya Kyaka
        • Kata ya Mushasha
        • Kata ya Kilimilile
        • Kata ya Mabale
        • Kata ya Bugorora
      • Tarafa ya Kiziba
        • Kata ya Bugandika
        • Kata ya Kitobo
        • Kata ya Buyango
        • Kata ya Ruzinga
        • Kata ya Bwanjai
        • Kata ya Gera
        • Kata ya Ishozi
        • Kata ya Ishunju
        • Kata ya Kanyigo
        • Kata ya Kashenye
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Kiuchumi
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Kudhibiti ukimwi
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayo Tekelezwa
    • Miradi Inayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha

HALMASHAURI YATOA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WAJASIRIAMALI WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVu

Posted on: September 5th, 2020

Na Mwandishi wetu.

Halmashauri ya wilaya ya Missenyi imeendelea kutekeleza lengo la kuboresha hali ya maisha ya wananchi kijamii na kiuchumi kwa kutoa mikopo kwa vikundi 23 kwa vijana, wazee na walemavu kwa kipindi cha robo ya nne ya mwaka wa fedha 2019/2020. Mikopo hiyo ni kutekeleza maelekezo ya Serikali ya kuhakikisha asilimia kumi ya mapato ya ndani yanatengwa kwa ajili ya kuwawezesha wajisiliamali wanawake, vijana na walemavu kutekeleza shughurizao za ujasiliamali wenye tija.

Katika hafla ya utoaji mikopo kwa vikundi vya wajasiriamali wanawake,vijana na watu wenye ulemavu iliyofanyika katika Ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya WIlaya ya Missenyi leo Septemba 5/2020 jumla ya Kiasi cha Tshs 82,750,000.00 zimekopeshwa kwa jumla ya vikundi 23 ikiwa ni vikundi 18 vya wanawake (Tsh 58,000,000.00), vikundi vinne vya vijana (Tsh 21,750,000.00) na kikundi kimoja cha watu wenye ulemavu (Tsh. 3,000,000.00). Mikopo hii inatarajiwa kurejeshwa na vikundi husika ndani ya mwaka mmoja  na haina riba.

Kwa mwaka wa fedha 2019/2020 Halmashauri ililenga kutoa mikopo isiyo na riba kwa vikundi vya wanawake, vijana na walemavu yenye thamani ya Tshs. 194,220,000.00. Hadi juni 2020, Halmashauri imetoa mikopo yenye thamani ya Tshs. 194,220,000.00 sawa na asilimia 100 ya lengo la mwaka.

Akisoma taarifa ya utoaji wa mikopo kwa vikundi, Afisa maendeleo ya jamii Bi. Beatrice Sanga amesema manufaa yanayotarajiwa baada ya kutoa mikopo hii ni pamoja na kuwezesha vikundi kupanua mitaji, kuongeza uzalishaji wa bidhaa mbalimbali zitakazo kidhi mahitaji ya soko na kuleta manufaa yaliyokusudiwa kwa walengwa. Manufaa mengine ni kuchochea utengenezaji na upatikanaji wa ajira kwa vijana, kuwaepusha wanufaika na vitendo hatarishi vinavyochochea mmomonyoko wa maadili na uvunjifu wa amani, ukuaji wa uchumi wa kaya na jamii na kupunguza umasikini.  Pia Halmashauri itaongeza mapato kupitia vyanzo vyake vinavyoelekeana na shughuri za wajasiliamali.

Bi Sanga ametaja changamoto ambazo zimekuwa zikijitokeza  katika utoaji wa mikopo ni pamoja na baadhi ya wakopaji kukosa uaminifu kwa kukiuka mikataba , vikundi kubadili matumizi ya fedha walizokopeshwa kinyume na maandiko waliyowasilisha wakati wa kuomba mikopo na mwitikio mdogo wa vijana kuanzisha miradi ya pamoja yenye tija na kuomba mikopo.

Nae Mkuu wa Wilaya ya Missenyi  Col. Denis Filangali Mwila ambaye pia ndiye aliyekuwa mgeni rasmi wakati wa hafla ya kukabidhi mikopo , amevitaka vikundi vilivyopokea mikopo hiyo hasa vijana kuitumia mikopo hiyo kwa lengo lililokusudiwa na kuonyesha mfano wa kuigwa kwa vijana wengine na si kuitumia mikopo hiyo kwa namna isiyo faa.

Ili kufanya zoezi la utoaji mikopo kwa vikundi liwe endelevu,  Halmashauri imeendelea kusimamia urejeshaji wa mikopo kwa vikundi vilivyonufaika kwa kufanya ufuatiliaji wa mara kwa mara na utoaji wa elimu kwenye vikundi husika ili watumie fedha kwa malengo yaliyokusudiwa. Hii itaondoa tatizo la vikundi kufanya matumizi ya fedha za mikopo yasiyoendana na malengo ya mikopo. Sambamba na hilo uhamasishaji umeendelea kufanyika ili vijana wajiunge kwenye vikundi na kuanzisha miradi yenye tija kusudi wapate sifa ya kuomba mikopo inayotolewa na Halmashauri.

Tarifa Kwa Umma

  • TAARIFA KWA UMMA JUU YA UFAFANUZI WA TAARIFA INAYOSAMBAA MITANDAONI KUHUSU BAADHI YA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI WILAYANI MISSENYI KUWAAGIZA WANAFUNZI VYUMA CHAKAVU June 03, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA JUU YA MAPOKEZI YA SHILINGI MILIONI 445 MWEZI MEI KUTOKA SERIKALI KUU May 13, 2025
  • JIMBO LA NKENGE LIMEFANIKIWA KUBADILISHWA JINA RASMI NA KUWA JIMBO LA MISSENYI. May 12, 2025
  • TANGAZO LA KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA WILAYANI MISSENYI April 14, 2025
  • Tazama zote

Habari mpya

  • NGO's ZAASWA KUTOKUKUBALIANA NA MASHARTI MAGUMU YA WAFADHILI

    June 26, 2025
  • MISSENYI YATIA SAINI MKATABA WA UJENZI SOKO LA KISASA BUNAZI

    June 20, 2025
  • MISSENYI YAPATA HATI SAFI MIAKA 10 MFULULIZO

    June 17, 2025
  • PONGEZI NA TUZO ZATOLEWA KWA WALIMU, SHULE NA KATA KWA UFAULU MWAKA 2024

    June 05, 2025
  • Tazama zote

Video

TUMEPATA HATI SAFI, TUJIPONGEZE
Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Sheria ndogo za Halmashauri

Tovuti Muhimu

  • Tovuti ya Mkoa Kagera
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Tovuti ya Serikali Kuu
  • Tovuti ya TAMISEMI

Watembeleaji walipo

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Missenyi

    Sanduku la Posta: 38 Kyaka - MISSENYI

    Namba ya Simu ya mezani: +255 28 298 2836

    Namba ya simu : +255 28 298 2836

    Barua pepe: ded@missenyidc.go.tz

Anuani zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki @2017 Wilaya ya Missenyi. Haki zote zimehifadhiwa